Jeremiah 6:1-6
Yerusalemu Imezingirwa Na Jeshi
1 a“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini!
Kimbieni kutoka Yerusalemu!
Pigeni tarumbeta katika Tekoa!
Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu!
Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini,
na uharibifu wa kutisha.
2 bNitamwangamiza Binti Sayuni,
aliye mzuri sana na mwororo.
3 cWachungaji pamoja na makundi yao
watakuja dhidi yake;
watapiga mahema yao kumzunguka,
kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
4 d“Jiandaeni kwa vita dhidi yake!
Inukeni tumshambulie mchana!
Lakini, ole wetu, mchana unaisha,
na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku,
na kuharibu ngome zake!”
6 eHivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma
kuzunguka Yerusalemu.
Mji huu ni lazima uadhibiwe,
umejazwa na uonevu.
Copyright information for
SwhKC