Jeremiah 6:1-6

Yerusalemu Imezingirwa Na Jeshi


1 a“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini!
Kimbieni kutoka Yerusalemu!
Pigeni tarumbeta katika Tekoa!
Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu!
Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini,
na uharibifu wa kutisha.

2 bNitamwangamiza Binti Sayuni,
aliye mzuri sana na mwororo.

3 cWachungaji pamoja na makundi yao
watakuja dhidi yake;
watapiga mahema yao kumzunguka,
kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”


4 d“Jiandaeni kwa vita dhidi yake!
Inukeni tumshambulie mchana!
Lakini, ole wetu, mchana unaisha,
na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.

5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku,
na kuharibu ngome zake!”

6 eHivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma
kuzunguka Yerusalemu.
Mji huu ni lazima uadhibiwe,
umejazwa na uonevu.
Copyright information for SwhKC